Friday, 13 April 2018

MO SALAH AVUNJA REKODI LIGI KUU UINGEREZA

Mo Salah ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa mwezi Machi katika ligi kuu nchini England.

Amekuwa mchezaji wa kwanza kuwahi kushinda tuzo hiyo mara 3 ndani ya msimu mmoja.

DROO YA UEFA NUSU FAINALI

Je Madrid Kuendeleza Ubabe Mbele Ya Bayern?
Mohamed Salah Dhidi Ya Waajiri Wake Wa Zamani

DROO YA EUROPA NUSU FAINALI

Nani Kuaga? Nani Kwenda Fainali?

Thursday, 12 April 2018

SIMBA YAENDELEZA DOZI BILA ANGALIA MTU USONI

Kikosi cha Simba kimezidi kujikita kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara(VPL) baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Mbeya City FC.

Mabao ya Simba yamefungwa na Emmanuel Anord Okwi, Asante Kwasi na John Bocco.

Mbeya City wamejipatia bao lao kupitia kwa Frank Ikobel na kuufanya mchezo umalizike kwa idadi hiyo ya mabao.

Simba wamefikisha alama 55 dhidi ya watani wao wa jadi Yanga walio na 47.

Mpaka sasa Simba imeshacheza jumla ya michezo 23 huku Yanga ikiwa na 22.

Vipi Kombe Litaenda Msimbazi Au Litaenda Jangwani?

KOCHA HANS VAN DER PLUIJM AMALIZANA NA AZAM FC


Kuna taarifa kwamba Kocha Mholanzi Hans van der Pluijm ameshamalizana na Azam FC ambayo ataanza kuinoa mara tu baada ya msimu huu kwisha.
Ligi imebakiza takribani mechi saba au nane kwa kila timu.

Inaelezwa kwamba kimyakimya Pluijm kamalizana na Azam FC.

"Kweli kocha amesaini mkataba wa miaka miwili na kila kitu safi, akimaliza msimu anaenda zake Azam FC," kilieleza chanzo.

Kwa sasa, Pluijm anainoa Singida lakini Yanga inaonekana ilipania kumpata Baada ya kuondoka kwa Kocha George Lwandamina ambaye amerejea kwao Zambia na kujiunga na Zesco tena.

Ingawa inaonekana kocha huyo asingependa kulizingumzia suala hilo mapema sana.

Kaa Karibu Zaidi Na Blog Yetu Kwa Taarifa Zaidi

Tuesday, 10 April 2018

Bodigadi wa Mayweather apigwa risasi Atlanta




Vyombo mbalimbali vya habari vimeripoti kuwa mtu mmoja anaedaiwa kuwa mmoja wa walinzi wa karibu wa bondia wa Marekani, Floyd Mayweather amepigwa risasi nje ya Hoteli ya Atlanta hapo jana asubuhi siku ya Jumatatu.

Mtandao wa habari za michezo wa TMZ Sports umeripoti kuwa kwamujibu wa taarifa za Polisi, risasi imetoka kwa mtu ambaye alikuwa kati ya moja ya magari matatu yaliyokuwa yamewasili nyuma ya hoteli ya InterContinental Buckhead majira ya saa 3 a.m. asubuhi siku ya Jumatatu.

Kwa mujibu wa chombo cha habari cha CNN kimeripoti kuwa mlinzi huyo ambaye jina lake halija fahamika amefikishwa kwenye Hospitali ya Grady Memorial kwaajili ya kupatiwa matibabu kufuatia risasi hiyo kumjeruhi mguuni na hali yake inaendelea vizuri.

Taarifa kutoka Polisi zinaeleza kuwa wanaamini bondia, Mayweather alikuwa sehemu ya msafara huo uliyoshambuliwa licha ya kutokuwa na uhakika kama yeye ndiye alikuwa mlengwa wa tukio hilo.

Hii ndio ratiba ya nusu fainali kombe la shirikisho

 

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limewataarifu wapenzi wa soka nchini kuwa michuano ya kombe ya Shirikisho (ASFC) kwa hatua ya nusu fainali inatarajiwa kuanza kutimua vumbi mnamo Aprili 20 na 21, 2018 kwa timu nne zilizoweza kufuzu nafasi hiyo.

Hayo yamewekwa wazi na Afisa Habari wa TFF, Cliford Mario Ndimbo wakati alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam na kusema nusu fainali ya kwanza itachezwa siku ya Ijumaa Aprili 20,2018 ikiwakutanisha Stand United ya Shinyanga watakaokuwa wenyeji wa Mtibwa Sugar ya Morogoro kwenye uwanja wa Kambarage Mkoani Shinyanga.

Aidha, Ndimbo amesema timu ya Singida United watawakaribisha JKT Tanzania kwenye nusu fainali ya pili itakayochezwa katika dimba la Namfua siku ya Jumamosi Aprili 21,2018.

Kwa upande mwingine, Ndimbo amesema washindi kwenye nusu fainali hizo watacheza mchezo wa fainali Mei 31, 2018.