Mo Salah ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa mwezi Machi katika ligi kuu nchini England.
Amekuwa mchezaji wa kwanza kuwahi kushinda tuzo hiyo mara 3 ndani ya msimu mmoja.
Lengo letu ni kukujuza Habari Zote Za Michezo Kitaifa na Kimataifa Tangaza nasi Leo call 0717827307.
Mo Salah ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa mwezi Machi katika ligi kuu nchini England.
Amekuwa mchezaji wa kwanza kuwahi kushinda tuzo hiyo mara 3 ndani ya msimu mmoja.
Kikosi cha Simba kimezidi kujikita kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara(VPL) baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Mbeya City FC.
Mabao ya Simba yamefungwa na Emmanuel Anord Okwi, Asante Kwasi na John Bocco.
Mbeya City wamejipatia bao lao kupitia kwa Frank Ikobel na kuufanya mchezo umalizike kwa idadi hiyo ya mabao.
Simba wamefikisha alama 55 dhidi ya watani wao wa jadi Yanga walio na 47.
Mpaka sasa Simba imeshacheza jumla ya michezo 23 huku Yanga ikiwa na 22.
Vipi Kombe Litaenda Msimbazi Au Litaenda Jangwani?
Kuna taarifa kwamba Kocha Mholanzi Hans van der Pluijm ameshamalizana na Azam FC ambayo ataanza kuinoa mara tu baada ya msimu huu kwisha.
Ligi imebakiza takribani mechi saba au nane kwa kila timu.
Inaelezwa kwamba kimyakimya Pluijm kamalizana na Azam FC.
"Kweli kocha amesaini mkataba wa miaka miwili na kila kitu safi, akimaliza msimu anaenda zake Azam FC," kilieleza chanzo.
Kwa sasa, Pluijm anainoa Singida lakini Yanga inaonekana ilipania kumpata Baada ya kuondoka kwa Kocha George Lwandamina ambaye amerejea kwao Zambia na kujiunga na Zesco tena.
Ingawa inaonekana kocha huyo asingependa kulizingumzia suala hilo mapema sana.
Kaa Karibu Zaidi Na Blog Yetu Kwa Taarifa Zaidi